Wednesday, August 28, 2013

GUARDIOLA NI BORA KULIKO MOURINHO - HOENESS.

RAIS wa klabu ya Bayern Munich, Uli Hoeness anadhani kuwa Pep Guardiola ameonyesha kwamba yeye ni kocha bora kuliko meneja wa Chelsea Jose Mourinho katika kipindi chake wakati akiwa Barcelona. Guardiola amekuwa na uhusiano wa mashaka na Mourinho wakati wote wakiwa nchini Hispania na maneno baina ya wawili hao yameibuka tena wiki hii wakati Mourinho alipohoji uwezo wa Guardiola kabla ya mchezo wao wa Super Cup kuashiria msimu mpya wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Hata hivyo, Hoeness anaamini kuwa uamuzi wa kumteua Guardiola kuwa mbadala wa Jupp Heynckes unaonyesha wazi kuwa nani ni kocha bora. Hoeness amesema makocha hao wawili wamekuwa wakipambana kuonyeshana nani mbabe nchini Hispania kwa msimu kadhaa ambayo wamekuwa huko na Guardiola ameongoza kwa mbali. Bayern Munich ambao ni mabingwa wa Ulaya watakwaana na Chelsea ambao ni mabingwa wa Europa League katika mchezo utakaochezwa Ijumaa jijini Prague.

No comments:

Post a Comment