Friday, August 23, 2013

MADRID YAMTENGEA BALE JEZI NAMBA 11.

KWA mujibu wa vyombo vya habari nchini Hispania, klabu ya Real Madrid imeweka fulana zenye jina la winga mahiri wa kimataifa wa Wales Gareth Bale sokoni baada ya mazungumzo ya uhamisho utakaoweka rekodi ya dunia na Tottenham Hotspurs kufikia mahali pazuri. Mazungumzo kati ya Madrid na Spurs kuhusiana na na suala la Bale yanaonekana kufikia sehemu nzuri lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 bado hajaondoka kwenda Bernabeu kukamilisha mazungumzo binafsi. Gazeti moja la michezo jijini Madrid lilichapisha picha katika mtandao wake unaoonyesha fulana ya Bale iliyopewa namba 11 ikiwa katika duka la vifaa vya michezo vya klabu hiyo kongwe nchini humo. Usajili wa mchezaji huyo ambaye amekuwa roho ya Spurs msimu uliopita umezua gumzo kubwa barani Ulaya kwasababu ya kutaka kuvunja rekodi ya usajili ya paundi milioni 80 iliyokuwa ikishikiliwa na Cristiano Ronaldo wakati alipohamia Madrid akitokea Manchester United mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment