Friday, August 23, 2013

BARCELONA YAMNASA SUAREZ.

KLABU ya Barcelona ya Hispania imetangaza kumnasa kinda Denis Suarez kutoka klabu ya Manchester City kwa ada ambayo haikuwekwa wazi. Mchezaji huyo mwenye miaka 19 alikuwa akitabiriwa kurejea Hispania kwa kipindi kirefu na sasa amesaini mkataba wa miaka na Barcelona ambapo ataanzia katika kikosi B cha timu hiyo. Suarez ambaye ni mchezaji wa nafasi ya kiungo aliibukia katika shule ya Celta Vigo lakini aliondoka na kutimkia City katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi mwaka 2011. Hata hivyo alishindwa kuitwa katika kikosi cha kwanza cha City pamoja na kuteuliwa kuwa mchezaji bora anayechipukia mwaka 2012 hivyo kuamua kujaribu kwingine.

No comments:

Post a Comment