Friday, August 23, 2013

WENGER AJIPANGA KUMSAJILI TENA FLAMINI.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anajipanga kufanya usajili wake mkubwa katika kipindi hiki cha usajili kwa kumrudisha kiungo wake wa zamani Mathieu Flamini. Flamini mwenye umri wa miaka 29 amekuwa akifanya mazoezi na Arsenal katika kipindi cha wiki mbili baada ya klabu yake ya AC Milan kushindwa kumuongeza mkataba mwishoni mwa msimu uliopita. Flamini aliondoka Arsenal na kujiunga na Milan miaka mitano iliyopita kama mchezaji huru lakini anaonekana kutaka kurejea katika klabu yake hiyo ya zamani kama mchezaji huru tena. Kwa mujibu wa mtandao wa Daily Mail wa Uingereza, Wenger ameonyeshwa kuridhishwa na juhudi za Flamini katika mazoezi na kufikiria kumpa mkataba ili kujaribu kuimarisha kikosi chake ambacho kimekuwa kikisumbuliwa na majeruhi katika siku za karibuni. Viungo wa klabu hiyo Mikel Arteta, Abou Diaby na Alex Oxlade-Chamberlain wote ni majeruhi hivyo kumfanya Wenger kukiri kuwa anahitaji kusajili mchezaji wa kiungo ili kujaribu kuziba nafasi hiyo katika kipindi hiki.
0000

No comments:

Post a Comment