Wednesday, August 28, 2013

MCHEZAJI AFARIKI UWANJANI ARGENTINA.

MCHEZA soka wa Ligi Daraja la Tatu nchini Argentina amefariki kwa shinikizo la damu wakati mechi. Klabu ya Deportivo Laferrere imesema kuwa mchezaji huyo aitwaye Hector Sanabria alianguka katika dakika ya 29 ya mchezo dhidi ya General Lamadrid jana ikiwa ni siku moja kabla ya kutimiza miaka 28 ya kuzaliwa kwake. Mwamuzi wa mchezo huo Hernan Mastrangelo ambaye aliahirisha mchezo huo alidai kuwa Sanabria hakuwa amegongana wala kuwa karibu na mchezaji yoyote wakati anaanguka. Shirikisho la Soka nchini Argentina limesema mechi zote za ligi za mwishoni mwa wiki zitatanguliwa na kusimama kwa dakika moja kwa ajili ya kutoa heshima kwa Sanabria.

No comments:

Post a Comment