Wednesday, August 28, 2013

MALAWI WAMSHITAKI KESHI KWA UBAGUZI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Malawi, Tom Saintfiet amesema Shirikisho la Soka la nchi hiyo limemshitaki FIFA kocha wa timu ya taifa ya Nigeria Steven Keshi. Hata ya Shirikisho hilo imekuja kufuatia Keshi kumwambia Saintfiet kwamba ni mtu mweupe anayepaswa kurejea nchini kwao Ubelgiji. Hatua ya makocha hao kurushiana maneno imekuja kufuatia Saintfiet kuonyesha wasiwasi wa usalama katika mji wa Calabar uliopo kusini mwa Nigeria ambao utatumika kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia baina ya nchi hizo mbili. Keshi akihojiwa katika kipindi cha Afrikan TV amesema anafikiri kocha huyo wa Malawi ni mpuuzi na sio mwafrika hivyo anapaswa kurejea nchini kwao, kauli ambayo imechukuliwa na Saintfiet kama ni ubaguzi.

No comments:

Post a Comment