Wednesday, August 28, 2013

DJOKOVIC, FEDERER WASONGA MBELE US OPEN.

MICHUANO ya wazi ya Marekani imeendelea kupamba moto ambapo Sam Stosur wa Australia amekuwa mchezaji wa kwanza wa viwango vya juu kuenguliwa mapema katika michuano hiyo baada ya kukubali kipigo kutoka kwa mchezaji kinda Voctoria Duval. Stosur anayeshika namba 11 katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanawake , ambae ni bingwa wa michuano hiyo mwaka 2011 alijikuta akipoteza mchezo huo wa kwanza kwa Duval mwenye umri wa miaka 17 kwa 5-7 6-4 6-4. Kwa upande mwingine nyota anayeshika namba moja katika orodha za ubora duniani kwa upande wanaume Novak Djokovic alifanikiwa kutinga mzunguko wa pili wa michuano hiyo kwa kumtandika Ricardas Berankis kwa 6-1 6-2 6-2. Bingwa mara tano wa michuano hiyo Roger Federer wa Switzerland naye alifanikiwa kusonga mbele kwa kumchapa Grega Zemlja wa Slovakia kwa 6-3 6-2 7-5.

No comments:

Post a Comment