Wednesday, August 28, 2013

PODOLSKI AINGIA KATIKA ORODHA YA MAJERUHI ARSENAL.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa Lukas Podolski atakaa nje ya dimba kwa kipindi cha wiki tatu baada ya mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani kuumia msuli katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Fenerbahce jana usiku. Podolski alitolewa kwa machela mapema katika kipindi cha pili ambapo Arsenal ilishinda kwa mabao 2-0 katika Uwanja wa Emirates na kufanikiwa kutinga katika hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 5-0 katika mechi za mikondo miwili walizokutana. Wenger pia alishuhudia kiungo Aaron Ramsey ambaye alifunga mabao yote mawili naye akitolewa kutokana na kuumia kigimbi wakati Jack Wilshere alipata tatizo la kifundo cha mguu katika dakika za mwisho wa mchezo huo. Wenger amesema Wilshere anaonekana hakuumia sana lakini Podolski ana uhakika kuwa atakosekana kwa siku 21 huku Ramsey akitegemewa kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na tatizo alilopata.

No comments:

Post a Comment