Tuesday, August 27, 2013

MBIA ATIMKIA SEVILLA KWA MKOPO.

KIUNGO mahiri wa klabu ya Queen Park Rangers-QPR, Stephane Mbia, amejiunga na klabu ya Sevilla kwa mkopo. Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Cameroon, mwenye umri wa miaka 27, sasa ataichezea klabu hiyo ya Hispania msimu huu wote. Mbia alijiunga na QPR, kutoka klabu ya Marseille mwaka uliopita, kwa mkataba wa miaka miwili, naye Joey Barton akajiunga na Marseille msimu huo kwa mkopo. Aliicheza QPR mechi 32, wakati klabu hiyo iliposhushwa daraja msimu uliopita. Mbia ni mchezaji wa Saba kuihama klabu hiyo kwa mkopo au kwa mkataba wa kudumu tangu waliposhushwa daraja. Katika miezi ya hivi karibuni, klabu hiyo imepoteza wachezaji wake Christopher Samba, Djibril Cisse, Jose Bosingwa, Loic Remy, Esteban Granero na Park Ji-sung. Mchezaji huyo kutoka Cameroon, alipigwa faini na QPR mwezi Mei mwaka uliopita, wakati alipotuma ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter akiashiria kuwa anataka kurejea Hispania na kuichezea klabu yake ya zamani

No comments:

Post a Comment