Sunday, September 22, 2013

CHISORA ANYAKUWA TAJI LA HEAVYWEIGHT BARANI ULAYA.

BONDIA Dereck Chisora wa Uingereza amefanikiwa kumtandika Edmund Gerber katika raundi ya tano na kufanikiwa kushinda taji la uzito wa juu la Ulaya katika pambano lililofanyika jijini London. Chisora ambaye ni mzaliwa wa Zimbabwe alioenekana kumzidi Gerber kuanzia raundi raundi ya tatu mpaka Mjerumani huyo aliposhindwa kabisa kuendelea kwenye raundi ya tano. Bondia huyo ambaye sasa ameshinda mapambano 18 kati ya 22 aliyocheza, amesema anataka kupigana kugombea taji la dunia kwa mara nyingine baada ya kupigwa kwa pointi na Vitali Klitschko. Kwa upande mwingine pambano la mabondia David Haye na Tyson Fury wote wa Uingereza lililokuwa lifanyike Septemba 28 limesogezwa mbele baada ya Haye kuumia kwa kujikata wakati akiwa mazoezini. Haye mwenye umri wa miaka 32 alijikata juu ya jicho lake wakati akiwa mazoezini hatua ambayo ilipelekea kushonwa nyuzi sita ambazo zitaondolewa baada ya siku sita mpaka saba.

No comments:

Post a Comment