Tuesday, September 24, 2013

MTUKUTU BALOTELLI AFUNGIWA MECHI TATU.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya AC Milan, Mario Balotelli amefungiwa mechi tatu na kamati ya Ligi Kuu nchini Italia baada ya kupewa kadi ya pili ya njano kwa kuzozana na mwamuzi katika mchezo dhidi ya Napoli Jumapili iliyopita. Balotelli ambaye alikosa penati na kufunga bao la kufutia machozi kwa timu yake katika dakika za majeruhi alipewa kadi ya pili ya njano na mwamuzi baada ya mpira kumalizika. Kwa kawaida mchezaji anayepewa kadi mbili za njano katika mchezo hukosa mechi moja lakini Balotelli amengezwa mechi mbili zaidi kwa tukio hilo la kumzonga mwamuzi hadharani. Mbali na adhabu hiyo ya Balotelli, Milan nao pia wamepewa adhabu ya kucheza bila mashabiki katika uwanja wao wa San Siro kwenye mechi nyingine ya ligi watakayocheza nyumbani kwasbabu ya mashabiki wao kufanya vitendo visivyo vya kiungwana kwa wenzao wa Napoli.

No comments:

Post a Comment