Friday, November 22, 2013

AYEW KUFANYIWA UPASUAJI.

KLABU ya Olympique Marseille imedai kuwa mshambuliaji wake nyota wa kimataifa wa Ghana Andre Ayew atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi miwili kutokana na majeraha ya mguu yanayomkabili. Ayew alipata majeraha wakati wa mchezo wa mkondo wa pili hatua ya mtoano ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia ambapo Ghana ilifungwa kwa mabao 2-1 na Misri Jumanne. Pamoja na kipigo hicho Ghana ilifuzu michuano hiyo itakayofanyika mwakani kwa jumla ya mabao 7-3 katika mechi mbili walizocheza na Misri. Nyota huyo ambaye anatarajiwa kufanyiwa upasuaji Jumatatu atakosa safari ya kwenda jijini London ambapo Marseille itakwaana na Arsenal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment