Friday, November 22, 2013

BURKINA FASO WAFIKISHA MALALAMIKO FIFA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA, limethibitisha kupata malalamiko kutoka Shirikisho la Soka la Burkina Faso kuhusiana na mchezo wao wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia ambapo nchi hiyo ilifungwa bao 1-0 na Algeria. Maofisa hao wa Burkinabe wameiandikia FIFA kulalamikia baadhi ya maamuzi yaliyofanywa na mwamuzi Badara Diatta wa Senegal wakati wa mchezo huo, maamuzi ambayo yalipelekea kukataliwa kwa bao lao katika kipindi cha kwanza. Shirikisho hilo pia limelalamikia kadi ya njano aliyopewa nahodha wa Algeria Madgid Bougherra wakidai kuwa alistahili kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi nahodha wa Burkinabe Charles Kabore katika eneo la hatari. Uamuzi wa FIFA unatarajiwa kuhusiana na tukio la mchezo huo unatarajiwa kutolewa Desemba 5, siku moja kabla ya ratiba kamili ya Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment