Thursday, November 21, 2013

BARCELONA KUWAKOSA MESSI NA VALDES MWAKA HUU.

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu nchini Hispania, Barcelona italazimika kucheza mechi zao nane zilizosalia kwa mwaka huu kuanzia mechi ya Jumamosi dhidi ya Granada bila ya mshambuliaji wake mahiri Lionel Messi na golikipa Victor Valdes. Messi yuko kitandani akiuguza msuli wa nyuma ya paja la mguu wake wa kushoto wakati Valdes ambaye amekuwa katika kiwango cha juu msimu huu naye amechanika msuli wa mguu wake wa kulia. Kama hiyo haitoshi, kuingo mchezeshaji wa timu hiyo Xavi Hernandez naye kuna hati hati ya kuukosa mchezo wa Jumamosi kutokana na majeraha ya msuli wa kigimbi na Jordi Alba naye bado yuko kitandani akijiuguza. Hata hivyo majeruhi hayawezi kuibabaisha klabu hiyo kutokana na historia ya nyuma kwani Valdes na Messi wamewahi kukosekana katika kikosi kwa muda unaofanana mwaka 2007 na timu hiyo kufanikiwa kushinda mechi 13 kati ya 16 walizocheza bila yao.

No comments:

Post a Comment