Thursday, November 21, 2013

GUARDIOLA APATA AHUENI BAADA YA BOATENG KUWA FITI TAYARI KWA DORTMUND.

KOCHA wa klabu ya Bayern Munich Pep Guardiola amepata habari njema kutoka katika meza ya madaktari wa timu hiyo kuelekea katika mchezo wa mwishoni mwa wiki dhidi ya mahasimu wao Borussia Dortmund. Madaktari wa timu hiyo wamemhakikishia kocha huyo kwamba beki wake tegemeo Jerome Boateng anatakuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo muhimu wa Bundesliga. Beki huyo wa kati aliumia kisigino wakati akiitumikia Ujerumani katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Uingereza ambao walishinda kwa bao 1-0 na Bayern walikuwa na hofu nyota huyo kukosekana katika mchezo huo wa Jumamosi. Hata Hivyo, Boateng mwenye umri wa miaka 25 alithibitisha kuwa atakuwepo katika mchezo huo utakaopigwa katika Uwanja wa Signal Iduna Park jijini Dortmund. Katika mchezo huo Bayern watakuwa wakisaka ushindi ili kuongeza pengo la alama kufikia nne katika msimamo wa Bundesliga wakati wapinzani wao watakuwa wakipambana ili kuhakikisha wanabakisha pengo la alama moja baina yao.

No comments:

Post a Comment