Thursday, November 21, 2013

ALVES AMFAGILIA RONALDO KUCHUKUA BALLON D'OR.

BEKI mahiri wa klabu ya Barcelona, Dani Alves amekiri kuwa mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo yuko katika kiwango bora kuliko hasimu wake katika tuzo za Ballon d’Or Lionel Messi na Franck Ribery lakini anafikiri kukosa taji lolote kwa Ronaldo msimu huu kunaweza kumgharimu kuikosa tuzo hiyo. Ronaldo mwenye umri wa miaka 28 amekuwa katika kiwango cha juu toka kuanza kwa msimu wa 2013-2014, akiwa amefunga mabao 24 katika mechi 17 alizocheza huku akifunga mabao mengine manne yaliyoiwezesha Ureno kukata tiketi ya michuano ya Kombe la Dunia 2014. Wakati akikiri kiwango kikubwa cha nyota huyo, Alves anaamini kuwa kukosa taji lolote kwa Madrid katika msimu wa 2012-2013 kutamuweka katika nafasi mbaya kwenye tuzo hizo. Alves amesema karata yake inakwenda kwa Messi au Ribery na kama sio Messi basi anayestahili tuzo hiyo ni Ribery kwasababu ameshinda kila na alikuwa mhimili muhimu kwa timu ya Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment