Thursday, November 21, 2013

ORODHA KAMILI YA TIMU 32 ZILIZOFUZU KOMBE LA DUNIA 2014.

URUGUAY imekuwa taifa la mwisho kukata tiketi ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2014 zitakazopigwa nchini Brazil baada ya kutoka sare ya 0-0 na Jordan katika mchezo wa mkondo wa pili hatua ya mtoano. Uruguay katika mchezo wa kwanza walipata ushindi wa mabao 5-0 na katika mchezo huo wa pili uliopigwa jijini Montevideo walitawala sehemu kubwa ya mchezo na walikaribia kufunga baada ya kichwa kilichopigwa na Diego Godin kugonga mlingoti. Nchi hiyo ya America Kusini ambao kwasasa wanakamata nafasi ya sita kwenye ubora wa viwango vya dunia walishinda taji hilo 1930 na 1950 na wakafika nusu fainali kwenye fainali zilizopigwa nchini Africa Kusini 2010. Orodha kamili ya timu 32 zitakazoshiriki michuano hiyo kwa upande wa bara la Afrika ni Algeria, Cameroon, Ghana, Ivory Coast, Nigeria, bara la Asia ni Australia, Iran, Japan na Korea Kusini wakati Ulaya itawakilishwa na Ubelgiji, Bosnia-Hercegovina, Croatia, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ugiriki, Italia, Uholanzi, Ureno, Urusi, Switzerland na Hispania. Nyingine ni Costa Rica, Honduras, Mexico na Marekani ambazo zinawakilisha nchi za Amerika Kaskazini, Kati na Caribbean huku bara la Amerika Kusini likiwakilishwa na Argentina, Brazil ambao ni wenyeji, Colombia, Ecuador, Chile na Uruguay.

No comments:

Post a Comment