Thursday, November 21, 2013

FIFA KUTUMIA SPRAY MAALUMU KATIKA MICHUANO YA KLABU BINGWA YA DUNIA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limepanga kutumia kutumia spray maalumu katika sehemu ya mstari wa ukuta kabla ya kupigwa adhabu kwenye michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia ili kuwarahisishia waamuzi. Katika taarifa yake FIFA imesema spray hiyo itatumika kwenye michuano hiyo itakayoanza kutimua vumbi December 11-21 nchini Morocco baada ya kufanyiwa majaribio kwenye michuano ya Kombe la Dunia kwa vijana chini ya miaka 17 na 20. Spray hiyo ambayo hupotea baada ya dakika moja itakuwa inapulizwa uwanjani kuchora mstari wa kupanga ukuta wa timu inayopigiwa adhabu, kitu ambacho kitaondoa kadi za njano ambazo hupewa mchezaji anayekaidi maamuzi ya mwamuzi ya kuonesha sehemu ya kuweka ukuta wa kulinda lango lao. Klabu bingwa ya dunia ya vilabu itazihusisha Bayern Munich ya Ujerumani, Atletico Mineiro ya Brazil, Guangzhou Evergrande ya China, Al Ahly ya Misri, Monterrey ya Mexico, Auckland City ya New Zealand na Raja Casablanca ya Morocco.

No comments:

Post a Comment