Wednesday, November 20, 2013

DESCHAMPS APEWA MIAKA MIWILI ZAIDI BAADA YA KUIWEZESHA UFARANSA KWENDA BRAZIL.

RAIS Shirikisho la Soka la Ufaransa, Noel Le Graet ametangaza kumuongeza mkataba kocha watimu ya taifa ya nchi hiyo Didier Deschamps ambao utamalizika mwaka 2016. Mkataba wa sasa wa Deschamps ulikuwa unamalizika baada ya fainali ya Kombe la Dunia lakini Le Graet alithibitisha kumuongeza mkataba kocha huyo baada ya ushindi dhidi ya Ukraine katika Uwanja wa Stade de France na kuwahakikishia nafasi ya kwenda Brazil. Akizungumza mara baada ya mchezo huo Le Graet amesema anamuunga mkono kocha huyo kwa asilimia 100 ndio wameona wamuongeze mkataba mwingine wa miaka miwili. Deschamps alisema mapema kwamba angeachia ngazi kama Ufaransa ingeshindwa michuano hiyo lakini ushindi wa mabao 3-0 waliopata ulitosha kuwahakikishia nafasi hiyo kwa jumla ya mabao 3-2 katika mechi mbili walizokutana na Ukraine.

No comments:

Post a Comment