Wednesday, November 20, 2013

MAJERUHI WAZIDI KUIANDAMA BARCELONA.

KLABU ya Barcelona imekumbwa na balaa la majeruhi kwa wachezaji wake jana baada ya nyota wake watatu kupata majeruhi wakati wakiwa katika majukumu ya kimataifa. Nyota hao walioumia ni pamoja na Xavi Hernandez ambaye vipimo vilionyesha amepata majeruhi ya msuli nyuma ya paja, Victor Valdes aliyetolewa katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Afrika Kusini na Cristian Tello aliyeumia kifundo cha mguu katika mazoezi. Golikipa Valdes ambaye amekuwa katika kiwango kizuri msimu huu alilazimika kutolewa nje katika kipindi cha pili kwenye mchezo huo ambao Hispania walichapwa kwa bao 1-0 katika Uwanja wa Soccer City jijini Johannesburg na nafasi yake kuchukuliwa na Iker Casillas. Shirikisho la Soka nchini Hispania-REEF limetoa taarifa katika ukurasa wa twitter wa timu ya taifa ya nchi hiyo kuwa wanahofu Valdes alichanika msuli katika kigimbi cha mguu wake wa kulia hivyo wanasubiri vipimo ili kujua ukubwa wa tatizo hilo. Nayo klabu ya Barcelona katika mtandao wake imethibitisha kutokuwa na uhakika wa kuwatumia kiungo wake Xavi na Tello katika mchezo wa La Liga Jumamosi dhidi ya timu ya Granada.

No comments:

Post a Comment