Wednesday, November 20, 2013

UFARANSA YAENDA BRAZIL KWA STAILI, RONALDO AMFUNIKA IBRAHIMOVIC.

TIMU ya taifa ya Ufaransa imefanikiwa kukata tiketi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil baada ya kufanikiwa kugeuza matokeo na kuiondosha Ukraine huku Cristiano Ronaldo naye akiihakikishia Ureno kwenda huko kwa kupiga mabao matatu peke yake. Timu hizo vigogo wa soka vya Ulaya zinaungana na Croatia, Ugiriki, Ghana na Algeria kuelekea katika fainali hizo zinazochezwa majira ya kiangazi mwakani baada ya kufanikiwa kushindwa mechi zao za mtoano za mkondo wa pili jana. Ufaransa wao waligeuza matokeo ya kufungwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza kwa kuibugiza Ukraine kwa mabao 3-0 yaliyofungwa na Mamadou Sakho, Karim Benzema na linguine la kujifunga la Oleg Gusey na kuifanya nchi hiyo kufuzu kwa jumla ya mabao 3-2. Kwa upande wa Ureno wao walifanikiwa kuigaragaza Sweden kwa mabao 3-2 na kufuzu kwa jumla ya mabao 4-2 katika mechi mbili za mtoano walizokutana.

No comments:

Post a Comment