Wednesday, November 20, 2013

ROBINHO AIPITA REKODI YA PELE.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Brazil, Robinho amefanikiwa kuifungia Brazil bao la ushindi akitokea benchi katika ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Chile na kumfanya nyota huyo kufikisha mabao tisa aliyowafunga wapinzani wao hao wa Amerika Kusini. Robinho ambaye sasa ameipita rekodi iliyoweka na Pele kwa kufunga bao moja zaidi yake dhidi ya Chile, aliitwa tena katika kikosi cha nchi hiyo mapema mwezi huu kwa ajili ya mechi mbili za kirafiki baada ya kukaa nje kwa kipindi cha miaka miwili. Brazil inatarajiwa kucheza mechi moja zaidi ya kirafiki dhidi ya Afrika Kusini jijini Johannesburg Machi mwakani kabla ya kocha Luis Filipe Scolari hajatangaza kikosi cha mwisho cha Kombe la Dunia. Fainali za Kombe la Dunia mwakani zinaandaliwa na Brazil ikiwa ni mara ya kwanza toka mwaka 1950 walipofanya hivyo.

No comments:

Post a Comment