Sunday, November 3, 2013

UZEMBE WASABABISHA PELLEGRINI KUMPIGA CHINI JOE HART.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini amesema golikipa namba moja wa timu hiyo Joe Hart anahitaji muda wa kupumzika baada ya kumuacha katika mchezo wao wa Jumamosi dhidi ya Norwich City. Hali hiyo imekuja kufuatia Hart mwenye umri wa miaka 26 kufanya makosa ya kizembe katika mechi za karibuni alizocheza hivyo kuigharimu timu hiyo. Akihojiwa Pellegrini na mtandao wa timu hiyo amesema jukumu lake ni kuangalia kila wiki mchezaji gani ni bora kwa ajili ya kucheza. Kocha aliendelea kudai kuwa Hart anahitaji mapumziko na yataweza kumsadia kwasababu amecheza katika kila mechi kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita na kila mchezaji hupitia kipindi kibaya. Amesema anachotakiwa kufanya Hart hivi sasa ni kujituma kwa bidii ili aweze kurejea katika kiwango chake na atakuwa pamoja nae katika kipindi chote.

No comments:

Post a Comment