Sunday, November 3, 2013

VIPIGO MFULULIZO VYAMFUKUZISHA KAZI RAVANELLI.

KLABU ya Ajaccio imemtimua kocha wake Fabrizio Ravanelli baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-1 nyumbani kutoka kwa Velenciennes katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Ravanelli ambaye ni nyota wa zamani wa kimataifa wa Italia alichukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo Juni mwaka jana lakini ameshindwa kufanya vyema toka kuanza kwa msimu huu hatua ambao imepelekea timu hiyo kushika nafasi ya pili kutoka mikiani katika msimamo wa Ligue 1. Mara baada ya mchezo huo Ravanelli alitangaza kuondoka na kudai kuwa mchezo huo waliopoteza ulikuwa wa mwisho kwake baada ya rais wa klabu hiyo Alain Orsoni kumtimua. Katika taarifa yake Orsoni amedai kuwa alikuwa hana njia nyingine zaidi ya kumtimua kocha huyo baada ya timu kupokea vipigo vinne mfululizo.

No comments:

Post a Comment