Sunday, November 3, 2013

VIJANA WAMEONYESHA UJASIRI - WENGER.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amekipongeza kikosi chake kwa kuonyesha ujasiri katika ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Liverpool jana. Arsenal ilitinga katika mchezo huo huku wakiwa wamepoteza mechi zao mbili za nyumbani moja ikiwa ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund na nyingine ya Kombe la Ligi dhidi ya Chelsea. Akihojiwa Wenger amesema ni muhimu kubadilika na kuwashawishi watu kwamba mnaweza kushinda mechi kubwa kama hiyo. Wenger aliendelea kudai kuwa kushinda mechi kubwa kama hiyo katika kiwango bora kama walivyocheza jana ni suala la umuhimu zaidi. Kocha huyo amesema safu yake ya ulinzi ilicheza kwa nidhamu kubwa na kuwanyamazisha nyota wa Liverpool kama Daniel Surridge, Luis Suarez, Steven Gerrard na Philipe Coutinho hivyo mabeki wanne waliocheza jana wanastahili pongezi. Arsenal itasafiri kuifuata Borussia Dortmund Jumatano ijayo na kufuatiwa na mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Manchester United katika Uwanja wa Old Traford mwishoni mwa wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment