Sunday, November 3, 2013

WILSHERE, GIBBS HATARINI KUIKOSA DORTMUND.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amebainisha kuwa wachezaji wake Jack Wilshere na Kieran Gibbs wako katika hatihati ya kukosa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borussia Dortmund Jumatano. Wilshere ameendelea kusumbuliwa na tatizo lake la kipindi kirefu la kifundo cha mguu lilosababisha kukosa mchezo dhidi ya Liverpool wakati Gibbs yeye alitolewa katika dakika ya 78 baada ya kuumia kwenye kigimbi. Wenger amebakia katika kiza juu ya mstakabali wa wachezaji hao majeruhi na kukiri kuwa hana uhakika kama watakuwa fiti kwa ajili ya mchezo dhidi ya Dortmund utakaofanyika huko Ujerumani. Arsenal imeongeza pengo la alama kileleni kufikia tano baada ya kuichapa Liverpool na Wenger ameonyesha kufurahishwa na kikosi chake kufuatia vipigo viwili mfululizo kutoka kwa Dortmund na Chelsea.

No comments:

Post a Comment