Sunday, November 3, 2013

BAYERN MUNICH YAFIKIA REKODI YA KUTOFUNGWA MECHI 36 ZA LIGI ILIYOWEKWA NA HUMBURG .

KLABU ya Bayern Munich jana ilipambana baada ya kuwa nyuma kwa bao moja katika mchezo dhidi ya Hoffenheim na kufanikiwa kushinda mabao 2-1 na kurejea kileleni mwa msimamo wa Bundesliga huku wakifikia rekodi ya kucheza mechi 36 za ligi bila kufungwa. Katika mchezo huo wenyeji Hoffenheim walifanikiwa kufunga bao la kuongoza mwishoni mwa kipindi cha kwanza kupitia kwa kinda Niklas Sule lakini Bayern walifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika tano baadae kupitia kwa Mario Mandzuki na kupelekea timu kwenda mapumziko zikiwa zimetoshana nguvu. Bao la pili la Bayern lilifungwa na Thomas Muller aliyemalizia pasi maridadi ya Franck Ribery na kuifanya timu hiyo kukaa kileleni kwa tofauti moja ya alama na Borussia Dortmund wanaoshika nafasi ya pili. Bayern haijapoteza mchezo wa ligi toka walipofungwa mabao 2-1 na Bayer Liverkusen Octoba mwaka jana na kama wakifanikiwa kushinda mchezo dhidi ya Augsburg mwishoni mwa wiki ijayo watakuwa wameipita rekodi hiyo iliyowekwa na Humburg miaka 30 iliyopita.

No comments:

Post a Comment