Sunday, November 3, 2013

UKAME WA MABAO HAUMSUMBUI MESSI.

KOCHA wa Barcelona, Gerardo Martino amesema mshambuliaji nyota wa timu hiyo Lionel Messi hana wasiwasi pamoja na kushindwa kufunga katika mechi za mechi za La Liga zilizopita. Alexis Sanchez alifunga bao pekee wakati Barcelona walipowafunga mahasimu wao wanaotoka mji mmoja Espanyol kwa bao 1-0 Ijumaa iliyopita na kuendeleza rekodi yao ya kutofungwa mechi 12 za ligi toka kuanza kwa msimu. Hii inakuwa ni mara ya kwanza kwa Messi toka Agosti mwaka 2011 kutofunga bao katika mechi nne za ligi. Martino amesema nyota huyo hana tatizo lolote pamoja na kushindwa kufunga na haoni kwanini watu wanafanya kitu hicho kuwa cha ajabu. Messi amefunga mabao 223 katika mechi 217 za ligi toka aanze kuitumikia Barcelona.

No comments:

Post a Comment