Sunday, November 3, 2013

MOURINHO AWAPONDA WACHEZAJI WAKE BAADA YA KIPIGO.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekikosoa kikosi chake kufuatia kipigo cha mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi ya Newcastle jana na kuongeza hakustahili chochote kutoka katika mchezo huo. Kama Chelsea ingepata ushindi katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Saint James Park wangeweza kukaa kileleni kwa muda lakini badala yake wamebakia katika nafasi ya pili mwa msimamo wa ligi hiyo wakiwa wamefungana alama 20 na Liverpool. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Mourinho amesema hakupenda kabisa mchezo waliocheza na walistahili kushindwa katika mchezo huo. Mourinho amesema walikuwa na nafasi nzuri za kufunga na kusawazisha lakini Newcastle walikuwa kimchezo zaidi kuliko wao ndio maana walistahili.

No comments:

Post a Comment