Monday, December 9, 2013

HAPATOSHI LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA.

WAKATI hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya ikielekea mwishoni wiki hii timu kadhaa zitaungana na Manchester United, Real Madrid, Paris Saint-Germain, Bayern Munich, Manchester City, Chelsea, Atletico Madrid na Barcelona katika hatua ya timu 16 bora. Timu zilizopo kundi A na D zitacheza mechi zake za mwisho kesho wakati makundi mengine yaliyobakia yatacheza mechi zao Jumatatu huku timu kadhaa zikihitaji ushindi ili kusonga mbele katika michuano hiyo. Katika kundi A Shakhtar Donetsk wanaweza kukata tiketi ya kusonga mbele kama wakifanikiwa kuifunga Manchester United ugenini wakati sare inaweza pia kuwavusha kama Bayer Leverkusen ikishindwa kuifunga Real Sociedad. Kwa upande wa kundi D Juventus itajihakikishia kuendelea kuwepo katika michuano hiyo kama wakishinda au kutoa sare dhidi ya Galatasaray jijini Instabul wakati kwa upande mwingine Galatasaray watasonga mbele kama wakifanikiwa kuchukua alama zote tatu kutoka Juventus.

No comments:

Post a Comment