Monday, December 9, 2013

DROGBA, EBOUE MATATANI KWA KUONYESHA FULANA KUMKUMBUKA NELSON MANDELA.

KAMATI ya nidhamu ya Shirikisho la Soka la Uturuki-TFF linatarajia kuwahoji nyota wawili wa kimataifa wa Ivory Coast wanaocheza klabu ya Galatasaray, Didier Drogba ba Emmanuel Eboue kufuatia kuonyesha ishara katika mechi ya kumkumbuka rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela aliyefariki dunia Alhamisi. Baada ya Galatasaray kushinda mabao 2-0 dhidi ya SB Elagizspor katika mchezo wa Kombe la Ligi Ijumaa, nyota hao wawili walivua fulana zao na kubakia na vesti zilizokuwa na ujumbe kuhusu Mandela. Mara baada ya Drgba kuvua fulana yake vesti aliyokuwa amevaa ndani ilikuwa na maandishi yaliyosema “Thank you Madiba” akimaanisha asante Madiba wakati vesti ya Eboue ilikuwa na maandishi yaliyosomeka “Rest in Peace Nelson Mandela” akimaanisha pumzika kwa amani Nelson Mandela. TFF linakataza kuonyesha fulana yoyote yenye ujumbe unaohusiana na mambo ya siasa wakari wa mechi ya soka.


No comments:

Post a Comment