Monday, December 9, 2013

WENGER ALIKATAA BAO LA KUSAWAZISHA LA EVERTON.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ameonyesha kutofurahishwa na bao la kusawazisha la Everton baada ya timu hiyo kushindwa kukaa kileleni kwa tofauti ya alama saba kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza. Bao la kusawazisha la Everton lililofungwa na Gerard Deulofeu katika dakika ya 84 liliifanya Everton kuchukua alama muhimu katika Uwanja wa Emirates baada ya pia ya kuwafunga Manchester United katikati ya wiki. Lakini Wenger ambaye pia hakufurahishwa na mchezo wa nguvu waliokuwa wakicheza Everton alisikitishwa na bao hilo kuruhusiwa baada ya kuonekana kuwa Romelo Lukaku alikuwa amezidi wakati akitengeneza nafasi ya kufunga bao hilo. Mbali na Lukaku kuzidi Wenger anaamini kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji pia alicheza faulo kwa beki wake Laurent Koscielny.

No comments:

Post a Comment