Monday, December 9, 2013

VURUGU BRAZIL, HELIKOPTA YATUA UWANJANI KUOKOA MAJERUHI.

MICHUANO ya Kombe la Dunia 2014 itakayofanyika nchini Brazil imeingia doa baada ya mashabiki watatu kuumizwa vibaya katika vurugu zilizotokea katika mchezo wa ligi ya nchi hiyo. Polisi wamedai kuwa mashabiki wa timu za Atletico Paraense na Vasco da Gama walikuwa wakipigana huku wakikimbia katika majukwaa katika Uwanja wa Catarina mara baada ya Atletico kufunga bao la kuongoza dakika ya 17 ya mchezo. 
Helikopta ya polisi ililazimika kutua uwanjani ili kumaliza vurugu hizo na kusaidia majeruhi kuwapeleka hospitali. Mchezo huo ulisimamishwa kwa saa moja kabla ya kuanza tena.

No comments:

Post a Comment