Monday, December 9, 2013

RATIBA YA KOMBE LA FA HADHARANI.

KLABU ya Arsenal imepangwa kucheza na wapinzani wao kutoka London ya Kaskazini, Tottenham Hotspurs katika mzunguko wa tatu wa michuano ya Kombe la FA. Kwa upande mwingine Manchester City wao watasafiri kuifuata Blackburn Rovers, Chelsea watakuwa ugenini kukwaana na Derby County wakati Manchester United wao watakuwa wenyeji wa Swansea. Mabingwa watetezi wa kombe hilo Wigan Athletic wataanza kampeni zao kwa kuikaribisha Milton Keynes Dons huku Liverpool wakimenyana wababe wao waliowafunga mabao 3-2 msimu uliopita timu ya Oldham au Mansfield. Mechi zingine za mzunguko huo zitakuwa kati ya West Bromwich dhidi ya Crystal Palace, Newcastle United dhidi Cardiff City na Norwich dhidi ya Fulham.

No comments:

Post a Comment