Friday, December 20, 2013

RUFANI YA WILSHERE YAGONGA MWAMBA.

CHAMA cha Soka nchini Uingereza-FA kimemfungia kucheza mechi mbili kiungo wa klabu ya Arsenal, Jack Wilshere baada ya kukutwa na hatia ya kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Manchester City. Tukio hilo lilitokea wakati Arsenal walipopata kipigo cha mabao 6-3 kutoka kwa City kwenye Uwanja wa Etihad Jumamosi iliyopita. Mwamuzi wa mchezo huo hakuliona tukio hilo lakini picha za video zilimuonyesha kiungo huyo akionyesha ishara hiyo ambapo pamoja na kukiri kosa hilo lakini Wilshere alidai kuwa adhabu aliyopewa ilikuwa kubwa. Wilshere atakosa mechi mbili za muhimu kutoka kwa mahasimu wao wa jiji la London timu ya Chelsea ambayo watacheza nayo Jumatatu na West Ham United Desemba 26 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment