Thursday, December 19, 2013

HATIMAYE OKWI AWASILI KUITUMIKIA YANGA.

HATIMAYE mshambuliaji Emmanuel Okwi amewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere -JNIA, Dar es Salaam jioni hii tayari kuanza kuutumikia Mkataba wake wa miaka miwili katika klabu ya Yanga. Okwi alitua kwa ndege ya RwandaAir Saa 9:55 jioni na kulakiwa na viongozi na mamia ya wapenzi kadhaa wa timu hiyo JNIA kabla ya kupakiwa kwenye gari ndogo alilokuwa akiendesha Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Kimataifa ya Yanga, Seif Ahmed na kuondoka. Mbali na Ahmed aliyekuwa akiendesha gari Okwi alikaa kiti cha nyuma sambamba na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Mussa Katabaro. Okwi alitokea geti la wageni maalum la JNIA na kusindikizwa na Polisi huku, umati wa mashabiki wa Yanga ukimshangilia na kumfanya atoke kwa taabu hadi kupanda gari.

No comments:

Post a Comment