Thursday, December 19, 2013

TANZANIA YAMALIZA MWAKA KATIKA NAFASI YA 120 VIWANGO VYA FIFA.

TANZANIA itamaliza mwaka 2013 ikiwa katika nafasi ya 120 katika viwango vipya vilivyotolewa na Shrikisho la Soka Duniani-FIFA mwezi huu. Katika miezi yote 12 Tanzania imekuwa ikipanda na kushuka mara kadhaa huku nafasi ya juu kabisa iliyofikiwa kwa mwaka huu ikiwa ni nafasi ya 109 walioshika Juni. Hispania imaliza mwaka kama vinara katika orodha hizo kwa mwaka wa sita mfululizo toka mwaka 2008 waliponyakuwa taji la michuano ya Ulaya wakizipiku nchi za Ujerumani waliopo nafasi ya pili, Argentina nafasi ya tatu, Colombia waliopo nafasi ya nne na Ureno wanaofunga orodha ya tano bora. Kwa upande wa Afrika, Ivory Coast wameendelea kuongoza kwa kushika nafasi ya 17 wakifuatiwa na Ghana wanaoshika nafasi ya 24, huku Algeria wakiwa nafasi ya 26, wakati mabingwa wa Afrika Nigeria wao wako katika nafasi ya 37 na tano bora kwa upande wa Afrika inafungwa na Misri waliopo nafasi ya 41.

No comments:

Post a Comment