Thursday, December 19, 2013

UNITED, CITY ZATENGANISHWA KOMBE LA LIGI.

KLABU ya Manchester United na Manchester City zimetenganishwa katika ratiba ya michuano ya Kombe la Ligi hatua ya nusu fainali. United ambao walifanikiwa kuibamiza Stoke City kwa mabao 2-0 jana usiku inatarajiwa kuchuana na Sunderland ambao waliiondosha Chelsea katika mchezo wa robo fainali. Kwa upande wa City ambao walitinga hatua hiyo baada ya kuifunga kirahisi Leicester, wanatarajiwa kuivaa West ham United ambayo iliondosha Tottenham Hotspurs kwa mabao 2-1. Mkondo wa kwanza mechi hizo unatarajiwa kuchezwa Januari 6 mwakani wakati mhi za mkondo wa pili zikitarajiwa kuchezwa wiki moja baadae.

No comments:

Post a Comment