Thursday, December 19, 2013

MMILIKI WA QPR AMNG'ANG'ANIA REDKNAPP.

MMILIKI wa klabu ya Queens Park Rangers, Tony Fernandes anataka kumuona Harry Redknapp akibakia kuwa meneja wa klabu hiyo kwa miaka mingi na ana uhakika wa kumbakisha pamoja na vilabu mbalimbali kumhitaji. Mashabiki wa klabu ya Tottenham Hotspurs wanaonekana kumtaka Redknapp kurejea kuinoa timu hiyo baada ya kutimuliwa kwa Andres Villas-Boas. Lakini Fernandes ana uhakika kuwa kocha huyo atabakia hapo kwa kipindi kirefu kijacho kwasababu anadhani ni mmoja wa makocha bora kabisa duniani. Fernandes amesema hakuna haja ya kuwa profesa ili uweze kutambua kuwa timu nyingo zilizopata mafanikio nchini Uingereza zimekuwa zikiongozwa na makocha waliokaa kwa kipindi kirefu kama Arsene Wenger wa Arsenal, Sir Alex Ferguson wa Manchester United na David Moyes aliyekuwa akiinoa Everton. Bilionea huyo aliendela kudai kuwa Redknapp ni mmoja wa makocha wa kiwangu cha juu na watu wengi wanamhitaji lakini anadhani ana furaha kufanya kazi naye.

No comments:

Post a Comment