Thursday, December 19, 2013

RIBERY ATEULIWA MCHEZAJI BORA BUNDESLIGA.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Bayern Munich, Franck Ribery ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa Ligi Kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga kufuatiwa kiwango bora alichokionyesha katika miezi 12 iliyopita. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye pia yuko katika orodha ya kugombea tuzo ya Ballon d’Or sambamba na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, imekuwa ni tuzo yake ya tatu baada ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na ile ya mchezaji bora wa Ulaya alizoshinda mapema mwaka huu. Ribery mwenye umri wa miaka 30 alishinda tuzo hiyo mbele ya mshambuliaji wa Borussia Dortmund Robert Lewandowski ambaye kuna tetesi naye akahamia Bayern katika kipindi cha usajili majira ya kiangazi. Toka mwaka huu uanze Ribery amefunga mabao 18 na kutoa pasi za mwisho zilizozaa mabao 20 katika mechi 44 alizocheza katika mashindano yote na kuisaidia Bayern kushinda mataji matatu kwa pamoja.

No comments:

Post a Comment