Thursday, December 19, 2013

MPUTU ATISHIA KUTOSHIRIKI CHAN.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC, Tresor Mputu ametishia kujitoa katika timu ya taifa ya nchi hiyo itakayoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani itakayofanyika nchini Afrika Kusini mwez ujao. Nyota mwenye umri wa miaka 28 anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe amesema hatashiriki michuano hiyo kama mamlaka husika na maofisa wa soka wa nchi hiyo hawatachukua hatua za makusudi ili kuimarisha hali ya kazi kwa wachezaji wanaocheza soka nyumbani. Akihojiwa Mputu amesema anadhani hawezi kwenda Afrika Kusini kwasababu wachezaji wanaocheza nyumbani hawaheshimiwi na kuna hakuna maelewano ndani ya timu hivyo hali hiyo inaathiri kazi yao. Kama wahusika wakiweka mambo sawa kabla ya michuano hiyo hakuna shaka kwamba ataliwakilisha taifa lake kwa mara nyingine.

No comments:

Post a Comment