Thursday, December 19, 2013

WILSHERE AKUBALI ADHABU YA FA.

KIUNGO mahiri wa klabu ya Arsenal, Jack Wilshere amekubali adhabu aliyopewa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA lakini atapinga adhabu ya kufungiwa mechi mbili aliyopewa. Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza alikuwa akituhumiwa kuonyesha ishara ya matusi kwa mashabiki wa Manchester City katika uwanja wa Etihad baada ya timu yake kupewa kipigo cha mabao 6-3 katika mchezo wa Ligi Kuu uliofanyika wiki iliyopita. Tukio hilo halikuonwa na mwamuzi wa mchezo huo lakini picha za video zilimuonyesha Wilshere akitoa ishara hiyo na FA kumpatia adhabu kwa sheria mpya ambayo huwaruhusu kufanya hivyo kama tukio halikuonekana na mwamuzi. Kesi yake inatarajiwa kusikilizwa Alhamisi na kama adhabu ikibaki hivyo nyota huyo anatarajiwa kukosa mechi mbili za Ligi Kuu ukiwem mchezo dhidi ya Chelsea Desemba 23 na mchezo dhidi ya West Ham United siku tatu baadae.

No comments:

Post a Comment