Thursday, December 19, 2013

UWANJA WA BILBAO NA ATLETICO KUGOMBEA UENYEJI WA EURO 2020.

SHIRIKISHO la Soka nchini Hispania, RFEF limethibitisha kuwa Uwanja mpya wa San Mames uliopo Bilbao na Uwanja wa la Peineta wa Atletico Madrid ndio viwanja vitakavyotumika kuwania kuandaa mechi za michuano ya Ulaya 2020. Katika taarifa yake RFEF imedai kuwa baada ya kupitia viwanja vyote vinne vilivyotuma maombi vikiwemo viwanja vya Cornella El Prat wa Espanyol na ule mpya wa Mestalla wa Valencia, wameumua kuchukua viwanja hivyo viwili vya Bilbao na Atletico. Viwanja vyote vilivyochaguliwa ba RFEF bado havijakamilika kutokana na kuwa katika matengenezo. Uwanja mpya wa San Mames ulifunguliwa Septemba mwaka huu lakini jukwaa moja bado lipo katika matengenezo ili uweze kufukia uwezo wake wa kuchukua mashabiki 53,000. Kwa upande wa Uwanja wa La Peineta wenyewe hautakuwa tayari mpaka 2016 ambapo ukikamilika utakuwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 70,000.hi ya mechi.

No comments:

Post a Comment