Thursday, December 19, 2013

RAJA YATINGA FAINALI KLABU BINGWA YA DUNIA, RONALDINHO AGEUKA LULU.

WENYEJI wa michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia, Raja Casablanca ya Morocco imefanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo baada ya kuwagaragaza mabingwa wa soka wa Amerika Kusini timu ya Atletico Mineiro ya Brazil kwa mabao 3-1. Wenyeji Casablanca ndio walioanza kupata bao la kuongoza kabla ya Mineiro kupitia kwa nyota wao Ronaldinho kusawazisha bao hilo lakini wenyeji walikuja juu na kuongeza bao lingine katika dakika ya 84 kwa njia penati huku Vivien Madibe akihitimisha ushindi huo kwa kufunga bao la tatu dakika za majeruhi. Mara baada ya mchezo huo wachezaji wa Raja walimvamia Ronaldinho aliyekuwa akirejea katika vyumba vya kubadilishia nguo, kumsalimia na kumuomba viatu vyake alivyokuwa akitumia katika mchezo huo pamoja na fulana aliyovaa. Wenyeji hao sasa watakwaana na mabingwa wa soka barani Ulaya, Bayern Munich katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo utakaochezwa Jumamosi jijini Marakech.

No comments:

Post a Comment