Wednesday, December 18, 2013

REUS ATAKA KUSHINDANA AUBAMEYANG ILI KUHAKIKISHA KAMA ANA KASI KULIKO USAIN BOLT.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi wa Ujerumani, Julian Reus amempa changamoto winga mahiri wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubemeyang kushindana naye katika mbio za mita 100 ili kuhakiki kama nyota huyo wa soka ana kasi kuliko Usain Bolt. Aubameyang ambaye amefunga mabao mabao tisa msimu huu katika Bundesliga alitumia muda wa sekunde 3.7 katika mita 30 alizokimbia mazoezini, muda ambao unaonekana ni wa kasi zaidi na alioutumia Bolt wakati akiweka rekodi ya dunia yam bio za mita 100 kwa sekunde 9.58 mwaka 2009. Jumamosi iliyopita nyota huyo wa kimataifa wa Gabon alitamba katika mazungumzo ya luninga huko Ujerumani kwamba ana kasi zaidi ya Bolt madai ambayo Reus anataka kuhakikisha kwa kushindana naye. Reus amesema alichozungumza Aubameyang katika luninga kinamkera ndio maana anataka kushindana naye ili kulinda heshima ya riadha.

No comments:

Post a Comment