Tuesday, December 24, 2013

WENGER ALIA KUNYIMWA PENATI.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anaamini kuwa timu yake ilistahili kupewa penati kwa asilimia 100 baada ya kupata sare ya bila ya kufungana na Chelsea katika Uwanja wa Emirates jana usiku. Kauli hiyo ya Wenger imekuja kufuatia winga wake Theo Walcott kuangushwa na Willian katika eneo la hatari dakika ya 36 lakini mwamuzi wa mchezo huo Mike Dean alikataa kuwa adhabu. Wenger anaamini kama mwamuzi angewapa penati hiyo hakuna shaka hali ya mchezo ingebadilika na kuweza kuibuka na alama zote tatu. Akihojiwa Wenger amesem hana shaka katika mawazo yake kwamba ile ilikuwa ni penati ya wazi lakini hajui kwanini mwamuzi aliwakatalia. Wakati huohuo meneja wa Chelsea Jose Mourinho alimnanga Wenger kuwa aache kulalamika sana kwani mchezo wa soka lazima watu wagusane hivyo haoni tatizo kama mwamuzi hakuona kosa lililofanywa na Willian.

No comments:

Post a Comment