Tuesday, December 24, 2013

MWAKANI NITATISHA ZAIDI - RONALDO.

MSHAMBUIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefunga mabao 69 katika kipindi cha miezi 12 iliyopita lakini nyota huyo anafikiri kuwa kuna vitu vizuri zaidi vinakuja. Ronaldo mwenye umri wa miaka 28 amevunja rekodi kadhaa mwaka huu lakini mwenyewe amedai kuwa anaweza kucheza kwa kiwango cha juu zaidi mwakani. Mbali na rekodi pamoja na tuzo mbalimbali alizoshinda mwaka huu nyota huyo pia amejumuishwa katika orodha ya mwisho ya wachezaji watakaogombea tuzo ya Ballon d’Or mwakani. Ronaldo pia aliibeba timu yake ya taifa ya Ureno kufuzu hatua ya mtoano ya michuano ya Kombe la Dunia kwa kufunga mabao yote kwenye ushindi wa mabao 4-2 waliopata dhidi ya Sweden Novemba. Lakini pamoja na hayo yote nyota huyo aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook kuwa mwaka 2013 ulikuwa mzuri kwake lakini mwaka ujao utakuwa mzuri zaidi.

No comments:

Post a Comment