Tuesday, December 24, 2013

PETROVA AJITOA AUSTRALIA OPEN.

MCHEZAJI nyota wa tenisi, Nadia Petrova wa Urusi amejitoa katika michuano ya wazi ya Australia inayotarajiwa kuchezwa mapema mwakani kufuatia kifo cha mama yake kilichotokana na ajali ya gari. Mama yake Petrova aitwaye Nadezhda Illyina alikuwa mwanariadha ambaye aliwahi kushinda medali ya shaba katika mbio za mita 400 kupokezana vijiti katika michuano ya olimpiki iliyofanyika jijini Montreal mwaka 1976. Mrusi mwenzake Maria Kirilenko ambaye anashika namba 19 katika orodha za ubora duniani naye amjitoa kutokana na majeruhi. Kujitoa kwa Petrova kunamaanisha kuwa Tsevetana Pironkova mwenye umri wa miaka 26 raia wa Bulgaria atachukua nafasi hiyo katika droo kubwa ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment