Tuesday, December 24, 2013

UFARANSA KUJIPIMA NGUVU MECHI TATU KABLA YA KWENDA BRAZIL.

TIMU ya taifa ya Ufaransa inatarajiwa kuchezwa mechi tatu za kimataifa za kirafiki kabla hawajaondoka kuelekea nchini Brazil kushiriki michuano ya Kombe la Dunia. Shirikisho la Soka la nchi hiyo limedai kuwa timu hiyo itacheza mchezao wake wa kwanza wa kirafiki huko Stade de France mei 27 huku michezo mingine ikichezwa katika miji ya Nice Juni mosi na Lille Juni 8. Majina ya timu watakazopimana nazo nguvu yanatarajiwa kutolewa mapema mwakani. Ufaransa imepangwa kundi F sambamba na timu za Switzerland, Ecuador na Honduras.

No comments:

Post a Comment