Friday, December 27, 2013

MURRAY ALA KICHAPO ABU DHABI.

MCHEZAJI nyota wa tenisi kutoka Uingereza Andy Murray amejikuta akikubali kipigo kutoka kwa Jo-Wilfried Tsonga wa Ufaransa katika michuano ya ya dunia ya tenisi inayofanyika jijini Abu Dhabi. Hiyo ni mara ya kwanza kwa Murray kurejea tena uwanjani toka alipofanyiwa upasuaji wa mgongo miezi mitatu iliyopita. Murray anayeshika nafasi ya nne katika orodha za ubora dunia na bingwa wa michuano ya Wimbledon alijikuta akifungwa seti 2-0 zenye alama za 7-5 6-3 na Tsonga nayeshika nafasi ya 10 katika orodha katika michuano hiyo ya maonyesho. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Murray alijitetea kuwa uwanja ulikuwa unafanya mpira kwenda kasi sana na kukiri kuwa Tsonga alikuwa katika kiwango kizuri kuliko yeye katika mchezo huo. Michuano inayofahamika kwa jina la Mubabala inatarajiwa kuendelea tena leo ambapo Rafael Nadal anayeshika namba moja atachuana na Mhispania mwenzake David Ferrer.

No comments:

Post a Comment